Jumapili, 18 Septemba 2016

Karibuni Vijana na Wadau mbalimbali wapenda maendeleo ya Kigamboni yetu pendwa... Ndani ya Ubalozi wa Vijana Kigamboni (UVIKI)kuna Aina nne (4) za uanachama ambazo ni:
1.Mwanachama muasisi
2.Mwanachama wa kawaida
3.Mwanachama wa heshima
4.Mwanachama mshiriki
Utaona pichani kama zilivyo orodheshwa ndani ya katiba kwa kuna mengi ya kunufaika unapojiunga na Ubalozi wa Vijana Kigamboni.. Kwa ushauri,taarifa,maoni,maswali n.k tafadhali usisite kuwasiliana nasi kwa anuani zetu.. Ahsante




Baadi ya waasisi wa Ubalozi wa Vijana Kigamboni wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu mpya wa wilaya ya Kigamboni na maafisa elimu wa wilaya ya Kigamboni..

Mwenyekiti wa Ubalozi wa Vijana Kigamboni akimkabidhi T-shirt ya chama mkuu mpya wa wilaya wa Kigamboni kama ishara ya kumpongeza kwa kazi nzuri ya kuleta maendeleo anayoifanya na kumpa ahadi kutoka kwa vijana wa Kigamboni ya kuwa naye bega kwa bega katika kuhakikisha Kigamboni inakua nuru itakayotizamwa duniani koyte 

Ubalozi wa Vijana Kigamboni ulipata bahati ya kuhudhiria kikao kilichoandaliwa na mkuu wa wilaya ya Kigamboni dhumuni ikiwa ni kukusanya maoni kutoka kwa watu mbalimbali yatakayoweza kusaidia kupandisha ufaulu wa wanafunzi ndani ya wilaya ya Kigamboni.. Kama Ubalozi wa Vijana Kigamboni tunapenda kutoa pongezi za dhati kwa mkuu wetu mpya wa wilaya kwa juhudi zake anazozionyesha katika kuleta maendeleo ya Kigamboni yetu pendwa na wazo lake chanya la kushirikisha jamii inayomzunguka kuweza kukabiliana na changamoto zinazorudisha nyuma Kigamboni yetu kimaendeleo







Jumatano, 14 Septemba 2016

Mwenyekiti wa muda bw.#Alfred Tembo akiweka saini yake kwenye katiba ya Ubalozi wa Vijana Kigamboni kama kuthibitisha kuikubaliana nayo... Mambo moto karibuni wadau tujumuike kwa pamoja kuleta fursa kwa vijana ili kuwa komboa kifikra na kiuchumi..
Madhumuni makuu ya Ubalozi wa Vijana Kigamboni kama inavyoelezwa na katiba..

Jumatatu, 12 Septemba 2016

KUZALIWA KWA UVIKI..


 Jumapili ya tarehe 11-09-2016 itabaki kua siku ya kukumbukwa na wanaharakati wa maendeleo ya vijana Kigamboni hii ni baaada siku hii mwenyezi mungu kuibariki na kwa uwezo  wake UBALOZI WA VIJANA KIGAMBONI(UVIKI) ikazaliwa rasmi.. Ndani ya ukumbi wa Kijiji beach waasisi walikutana na kuweza kupitisha azimio la pamoja la kupitisha katiba itakayoongoza UVIKI kusonga mbele.. Karibuni vijana wa Kigamboni tuungane pamoja maana umoja na mshikamano ndio nguvu yetu

Jumanne, 6 Septemba 2016

KATIBA TOLEO LA KWANZA

Ubalozi wa Vijana Kigamboni tunamshukuru mungu kwa kuweza kutusimamia mpaka tukafanikiwa kulitimiza hili.. Safari inaanza huyu tukiomba mungu atunyooshee mikono yake tukufanyia wepesi kwa mambo mazuri yote yatakayo leta maendeleo kwa vijana wa Kigamboni na jamii inayomzunguka kwa ujumla.. MUNGU ibariki Tanzania, MUNGUibariki UVIKI

Utengenezaji wa katiba

.. kama inavyoonekana pichani baadhi ya waasisi wa Ubalozi wa Vijana Kigamboni(UVIKI) wakiwa katika mjadala mzito wa kutengeneza katiba sahihi itakayoweza kuwaongoza ipasavyo katika kuleta maendeleo ya vijana ndani ya kigamboni yetu pendwa..