SAFARI NI SAFARI INGAWA SI WOTE MTAFIKA MKONO WAKO MUNGU UENDELEE KUSHIKIRIA UVIKI NA WATU WAKE ILI WAWEZE KUFANYA MAPINDUZI YA FIKRA NA UCHUMI KWA JAMII NA VIJANA WA KIGAMBONI.
HISTORIA
FUPI YA UBALOZI WA VIJANA KIGAMBONI (UVIKI).
UBALOZI WA VIJANA KIGAMBONI (UVIKI) ni
kikundi cha kijamii kilichoanzishwa katika Wilaya ya Kigamboni,Kikundi hiki
kilianzishwa ili kuleta mapinduzi ya kifikra na kiuchumi kwa vijana na jamii
kwa ujumla pia kurudisha umoja na mshikamano baina ya kijana kwa kijana na
kijana kwa jamii ndani ya Kigamboni na nje ya Kigamboni.
ILIPOTOKA
Wazo la kuanzisha umoja huu lilitokana na harakati
za kuanzisha chama cha mpira wa miguu Kigamboni katika uwanja wa machava
Kigamboni,katika harakati hizo za kuanzisha chama cha mpira kulikuwa na
wanaharakti wengi sana wakiwemo,mwalimu bendera,Ramadhani shauritanga,deo lucas,Rashid,Mude,metusela,mecky,Tembo,Thabit
na wengine wengi
Hapo ndipo baadhi ya wanaharakati walipo hamua
kufanya jambo moja kwa mustakabari wa Kigamboni nzima si kwa michezo tu bali
katika Nyanja zote,wanaharakati hao wakiwemo Rashid.A.Rashid,Mecky
Michael,Alfred.K.Tembo,Ladislaus.S.Mude,Shilla Hamis,Salum Said,Metusela
Obedi,Thabit Molly na Kennedy Gimba.
Kwa pamoja walifanya kikao chao cha kwanza katika
uwanja wa machava kikao hicho walikiita KIKAO
WIMA (yaani walisimama na kufanya mazungumzo).katika kikao hicho mawazo
yalikuja mengi sana na majina mbalimbali juu ya kikundi husika,lakin jina moja
tu ndilo lililo kubaliwa na kupitishwa na lilipendekezwa na mwanaharakati
Alfred Tembo,jina hilo ni ubalozi wa vijana Kigamboni(Uviki).
Dhumuni kuu lilikuwa sisi tuwe mabalozi na
wawakilishi wa vijana wa Kigamboni ndani na nje ya Kigamboni.tukiamini kuwa
Kigamboni ina fursa nyingi ambazo vijana wake hawafaidiki nazo.
Ndugu Rashid.A.rashid alilichukua wazo hilo mpaka
kwa Ndugu Ramadhani Shauritanga ili kupata njia ya kuanzia ndipo Ndugu
Ramadhani kwa kutambua umuhimu wa jambo hili akaamua kutupa muongozo wa katiba
wa Chama Cha Vijana Kigamboni (Chaviki),ndugu Ramadhani alikuwa ni katibu wa
chama hicho,na alitusihii tuangalie mapungufu ambayo yaliwafanya wao kushindwa
kuendelea na umoja wao huo.
Tulianza vikao mara moja katika chumba cha Ndugu
Rashid.A.Rashid kwa kuichambua katiba hile ya Chaviki na kuangalia mapungufu yao,hakika safari
ilikuwa ngumu na yenye changamoto nyingi zikiwemo za muda,pesa na wengine
kuishia njia kutokana na ugumu uliyopo.
Hakika Mungu alitusimamia ipasavyo kwa kuwa alijua
kuwa tuna nia ya kweli ya kuifikisha Kigamboni sehemu inayostaili kufika.
Tulionelea hatuwezi kuendesha chama au kuandaa
katiba tukiwa na jinsia moja ndipo tulipo kubaliana na kufanya maamuzi ya
kuunganisha nguvu na mawazo na jinsia nyingine, ndipo walipo kuja wanaharakati
wa kike,Salome John,Sakina Athumani,Jesca Na Farida.J.Mtoto na kutimia timu ya watu kumi
na tatu.
Kwa umoja wetu tulipambana vya kutosha kufanikisha
kuipata katiba ya UVIKI, OFISI YA UVIKI, WALEZI NA WADHAMINI,bila kuwasahau
WANACHAMA WA UVIKI,pia tukiwa tunaendelea na mchakato wa USAJILI na sasa upo
katika ngazi ya kitaifa tushamaliza ngazi ya wilaya.
Tulianza wengi na wengine kuishia njian kutokana na
changamoto mbalimbali za kijamii.
Bodi ya waasisi wa ubalozi wa vijana Kigamboni
inawashukuru wote waliochangia kwa kiasi kikubwa kuisaidia kwa kipindi chote
kigumu cha mchakato wa kuusimamisha umoja huu.